Ufunuo kupitia Yesu
Kristo, ambao Mungu alimpa, kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima
yatendeke upesi.
Nazani kama ni
wafuatiliaji wazuri wa hile historia ya Mussa rafiki yangu kipenzi
aliyechaguliwa na Bwana Mungu wetu aliye juu mbinguni, Basi leo hii tutaanza na
historia hii ya ndugu yetu Mpenzi Yohana niliyekutana nae alfajiri ya leo
mida ya saa 04:08 ikiwa ni tarehe
14.05.2015 ilikuwa ni baada ya kumaliza kuimba nyimbo za Tenzi za Rohoni,
ambayo ni Tenzi namba 103. Kaa Nami, Tenzi namba 23. Ni Salama Rohoni Mwangu,
Tenzi namba 64. Ujaribiwapo, Sifanye Dhambi, Tenzi namba 121. Liko Lango Moja Wazi. Kiukweli kwa upande wangu,
ulikuwa ni usiku mzuri sana, kwani niliona Malaika wakishangilia kwa furaha,
huku Roho Takatifu aliyopo ndani yangu akifurahi hadi kifua kilikuwa kinaniuma,
kwa maana ungefanikiwa kushiriki katika uwepo uwo, lazima ungenena yakwamba;
“Roho za Bwana zipo ndani yetu”. “Kwa
Mungu, mwenye hekima peke yake, kuwe na utukufu kupitia Yesu Kristo milele.
Amina.
Naye alimtuma Malaika
wake na kupitia yeye akautoa kwa njia ya ishara kubwa kwa mtumwa wake Yohana,
aliyetoa ushahida kuhusu neno ambalo Mungu alitoa na kuhusu ushaidi ambao Yesu
Kristo alitoa, naam, kuhusu mambo yote aliyoyaona. Mwenye furaha ni yeye
anayesoma kwa sauti na wale wanaosikia maneno ya unabii huu, na wanaoshika
mambo yaliyoandikwa kwenye Biblia Takatifu ya neno la Mungu; kwa maana wakati
uliowekwa uko karibu.
Kisha akasema; (Na
muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na
aliyekuwako na anayekuja, na kutoka kwa zile roho saba zilizo mbele ya kiti
chake cha ufalme, na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,” “ Mzaliwa wa
kwanza kutoka kwa wafu,” na “Mtawala wa wafalme wa dunia”.
Kwake yeye
anayetupenda na aliyetufungua kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake mwenyewe.
Paulo, mtume wa
Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu kulingana na ahadi ya uzima ulio katika
muungano na Kristo Yesu, Kwa Temotheo, mtoto mpendwa;
Na kuwe na fadhili
zisizostahiliwa, rehema, amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
Paulo, Anamaliza kwa
kusema; “Lakini ujue jambo hili, ya kwamba katika siku za mwisho kutakuwa na
nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye
kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru,
wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa
asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali,
wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi,
wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu wakiwa
na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakizikana nguvu zake; nawe geukia
mbali kutoka kwa hao. Kwa maana kutoka kwa watu hao huinuka wale watu
wanaojiingiza kwa ujanja katika nyumba na kuwachukua mateka wanawake walio
dhaifu ambao wamelemewa na mizigo ya dhambi, wanaoongozwa na tamaa za namna
mbalimbali, wakijifunza sikuzote na bado hawawezi kamwe kufikia ujuzi sahihi
juu ya kweli.
Kwa hiyo, zikimbie
tama zinazotukia ujanani, lakini fuatilia uadilifu, imani, upendo, amani,
pamoja na wale wanaomwita Bwana kutokana na moyo safi.
Hapa, Yesu
Kristo naye akafungua kinywa chake na kuanza kunifundisha “kuwafundisha”,
akisema:
“Wenye furaha ni wale
wanaotambua uhitaji woa wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
“Wenye furaha ni wale
wanaoombeleza, kwa kuwa watafarijiwa.
“Wenye furaha ni wale
walio na tabia-pole, kwa kuwa watarithi dunia.
“Wenye furaha ni wale
walio na njaa na walio na kiu kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa watashibishwa.
“Wenye furaha ni wale
walio na rehema, kwa kuwa wataonyeshwa rehema.
“Wenye furaha ni wale
walio safi moyoni, kwa kuwa watamwona Mungu.
“Wenye furaha ni wale
wanaofanya amani, kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’
“Wenye furaha ni wale
ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
“Wenye furaha ni
ninyi wakati watu wanapowashutumu na kuwatesa na kusema kwa uwongo kila namna
ya jambo baya juu yenu kwa ajili yangu. Shangilieni na kuruka kwa shangwe, kwa
kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa
manabii waliokuwa kabla yenu.
“Ninyi ndio chumvi ya
dunia; lakini chumvi ikipoteza nguvu zake, ladha yake itarudishwaje? Haitumiki
tena kwa kitu chochote bali ni ya kutupwa nje ili ikanyagwe-kanyagwe na watu.
“Ninyi ndio nuru ya
ulimwengu. Jiji haliwezi kufichwa likiwa limesimama juu ya mlima. Watu huwasha
taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa,
nayo huangazia watu wote waliomo ndani ya nyumba. Vivyo hivyo achene nuru yenu iangazie
mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mazuri na kumpa utukufu Baba yenu
aliye mbinguni.
“Yeye anayetoa
ushahidi juu ya mambo haya na asema, ‘Ndiyo; mimi ninakuja upesi.’”
“Amina! Njoo, Bwana
Yesu.”
Fadhili
zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe pamoja na watakatifu.
Ndugu zangu yatupasa tumrudie Bwana Mungu wetu
JibuFuta