Alhamisi, 14 Mei 2015

TAMAA, UJANANI. NYAKATI ZA HATARI.



 
Nimeokoka Nampenda Mungu
Ufunuo kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa, kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima yatendeke upesi.

Nazani kama ni wafuatiliaji wazuri wa hile historia ya Mussa rafiki yangu kipenzi aliyechaguliwa na Bwana Mungu wetu aliye juu mbinguni, Basi leo hii tutaanza na historia hii ya ndugu yetu Mpenzi Yohana niliyekutana nae alfajiri ya leo mida  ya saa 04:08 ikiwa ni tarehe 14.05.2015 ilikuwa ni baada ya kumaliza kuimba nyimbo za Tenzi za Rohoni, ambayo ni Tenzi namba 103. Kaa Nami, Tenzi namba 23. Ni Salama Rohoni Mwangu, Tenzi namba 64. Ujaribiwapo, Sifanye Dhambi, Tenzi namba 121. Liko  Lango Moja Wazi. Kiukweli kwa upande wangu, ulikuwa ni usiku mzuri sana, kwani niliona Malaika wakishangilia kwa furaha, huku Roho Takatifu aliyopo ndani yangu akifurahi hadi kifua kilikuwa kinaniuma, kwa maana ungefanikiwa kushiriki katika uwepo uwo, lazima ungenena yakwamba; “Roho za Bwana zipo ndani yetu”.  “Kwa Mungu, mwenye hekima peke yake, kuwe na utukufu kupitia Yesu Kristo milele. Amina.
Naye alimtuma Malaika wake na kupitia yeye akautoa kwa njia ya ishara kubwa kwa mtumwa wake Yohana, aliyetoa ushahida kuhusu neno ambalo Mungu alitoa na kuhusu ushaidi ambao Yesu Kristo alitoa, naam, kuhusu mambo yote aliyoyaona. Mwenye furaha ni yeye anayesoma kwa sauti na wale wanaosikia maneno ya unabii huu, na wanaoshika mambo yaliyoandikwa kwenye Biblia Takatifu ya neno la Mungu; kwa maana wakati uliowekwa uko karibu.
Kisha akasema; (Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja, na kutoka kwa zile roho saba zilizo mbele ya kiti chake cha ufalme, na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,” “ Mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,” na “Mtawala wa wafalme wa dunia”.
Kwake yeye anayetupenda na aliyetufungua kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake  mwenyewe.
Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu kulingana na ahadi ya uzima ulio katika muungano na Kristo Yesu, Kwa Temotheo, mtoto mpendwa;
Na kuwe na fadhili zisizostahiliwa, rehema, amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
Paulo, Anamaliza kwa kusema; “Lakini ujue jambo hili, ya kwamba katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu wakiwa  na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakizikana nguvu zake; nawe geukia mbali kutoka kwa hao. Kwa maana kutoka kwa watu hao huinuka wale watu wanaojiingiza kwa ujanja katika nyumba na kuwachukua mateka wanawake walio dhaifu ambao wamelemewa na mizigo ya dhambi, wanaoongozwa na tamaa za namna mbalimbali, wakijifunza sikuzote na bado hawawezi kamwe kufikia ujuzi sahihi juu ya kweli.
Kwa hiyo, zikimbie tama zinazotukia ujanani, lakini fuatilia uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na wale wanaomwita Bwana kutokana na moyo safi.
                                Hapa, Yesu Kristo naye akafungua kinywa chake na kuanza kunifundisha “kuwafundisha”, akisema:
“Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji woa wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
“Wenye furaha ni wale wanaoombeleza, kwa kuwa watafarijiwa.
“Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watarithi dunia.
“Wenye furaha ni wale walio na njaa na walio na kiu kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa watashibishwa.
“Wenye furaha ni wale walio na rehema, kwa kuwa wataonyeshwa rehema.
“Wenye furaha ni wale walio safi moyoni, kwa kuwa watamwona Mungu.
“Wenye furaha ni wale wanaofanya amani, kwa kuwa wataitwa ‘wana wa Mungu.’
“Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
“Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanapowashutumu na kuwatesa na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo baya juu yenu kwa ajili yangu. Shangilieni na kuruka kwa shangwe, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.
“Ninyi ndio chumvi ya dunia; lakini chumvi ikipoteza nguvu zake, ladha yake itarudishwaje? Haitumiki tena kwa kitu chochote bali ni ya kutupwa nje ili ikanyagwe-kanyagwe na watu.
“Ninyi ndio nuru ya ulimwengu. Jiji haliwezi kufichwa likiwa limesimama juu ya mlima. Watu huwasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa, nayo huangazia watu wote waliomo ndani ya nyumba. Vivyo hivyo achene nuru yenu iangazie mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mazuri na kumpa utukufu Baba yenu aliye mbinguni.
“Yeye anayetoa ushahidi juu ya mambo haya na asema, ‘Ndiyo; mimi ninakuja upesi.’”
“Amina! Njoo, Bwana Yesu.”
Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe pamoja na watakatifu.  

Maoni 1 :

  1. Ndugu zangu yatupasa tumrudie Bwana Mungu wetu

    JibuFuta