Alhamisi, 14 Mei 2015

KUJIPAMBA. CHOMBO DHAIFU. KUJITETEA


Wakristo wote lazima wawe wahudumu


Mpendwa, mimi nasali kwamba uwe ukiendelea vema na kuwa na afya njema katika mambo yote, kama vile nafsi yako inavyoendelea vema. Kwa maana nilishangilia sana wakati akina ndugu walipokuja na kutoa ushahidi kuhusu kweli ambayo wewe unashika, kama vile unavyoendelea kutembea katika kweli. Sina sababu nyingine kubwa zaidi ya kuwa na shukrani kuliko mambo haya, kwamba niwe nikisikia ndugu zangu wanaendelea kutembea katika kweli. Mpendwa, unafanya kazi ya uaminifu kwa yoyote unayofanya kwa ajili ya akina ndugu, tena walio wageni, ambao wametoa ushahidi kuhusu upendo wako mbele ya kutaniko. 

Tafadhali  uishughulikie safari ya hawa watu kwa namna inayomfaa Mungu. Kwa maana hata manabii wa kale walisafiri kwa ajili ya jina lake, bila kuchukua kitu chochote kutoka kwa watu wa mataifa. Kwa hiyo, sisi tuna wajibu wa  kuwakaribisha watu wa namna hiyo, ili tuwe wafanyakazi wenzi katika kweli.
Amina.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni